Monday, June 22, 2015

SOMO: HAZINA ILIYOFICHWA NDANI YA MBEGU YA NENO LA MUNGU

Pastor Frank Andrea akifundisha katika ibada ya Ufufuo na Uzima Arusha






UTANGULIZI

Isaya 45:1-3

Mungu anasema nitakwenda mbele yako naminitakupa hazina za gizana na mali zilizo fichwa za mahali pa siri. Kuna vitu vipo vimefichwa za mahari pa siri ambavyo Bwana anahaidi atatupatia, Ni muhimu kujua kunavitu vipo ambavyo havionekani lakini Mungu amekuandalia wewe. Hata wakati wa uumbaji kunavitu Mungu alkuwa anavitaja lakini havikuako, Mwanzo 1:1-2, Mungu aliumba dunia na vyote kwa Neno. Kwa maneno mengine ukivichukua vitu vyote na kuviludisha viliko toka vitarudi ndani ya Neno la Mungu. Kitabu cha Yohana 1:1-5 kinasema vitu vyote viliubwa kwa Neno na Ndani ya huyo Neno ndimo mlimokuwepo uzima,,
Neno ni nini?
Kwenye maandiko Matakatifu yaani Bilblia emeeleza Neno kwa namna mbili
       i.            YESU
     ii.            MBEGU

NENO KWA MAANA YA YESU
YESU ni Neno Yohana1:1-4. Neno lilikuwa kinywani mwa MUNGU. Ukikusanya vituvyote virudi kwenye hasiri yake vyote vitarudi kwenye Neno. Huyu Neno kazi yake ilikuwa ni kumtia nuru kila mmoja ulimwenguni. Yohana1:14 inasema naye Neno akavaa mwili tukauona utukufu wake kama wa mwana pekee wa Mungu ambaye alikuwa ni Yesu.
NENO KWA MAANA YA MBEGU
Kitabu Luka 8:11 kinaeleza vizuri kuwa mbegu ni Neno la Mungu. kwa maneno mengine unaweza kusema ndani ya Mbegu ndimo mlimokuwepo uzima. Kwa mfano ukiwa na mbegu ya parachichi ndani yake kuna mapori ya maparachichi. Ukiwa na mbegu ya mchungwa ndani yake kuna mapori ya michungwa. Iliuendane na Mungu lazima ujifunze kuona kama yeye anavyoona..
Utaona Yesu anatoa mfano wa mbegu Luka 8:4-8, Yesu alikuwa anazungumzia Mbegu kama neno la Mungu na mahari pa kupanda kama aina za mioyo ya watu ambao wanalisikia Neno la Mungu.  Aina za mahari pa kupanda mbegu
       i.            Njiani : moyo njia ni moyo ambao mtu analisikia Neno la Mungu lakini  anafungua moyo wake na kuruhusu mambo mabaya kuingia kwake. Na ndege huja kuula
     ii.            Mwamba: moyo mwamba ni moyo usio tayari kupokea chochote, ulisikiliza Neno lakini hulizuia lisiingie ndani yake.
  iii.            Udongo wa Miiba: moyo miiba ni moyo buzy, moyo ambao unasongwa na mambo mengi ya duniani, kama kazi, maisha n.k
  iv.            Udongo mzuri:mbegu iliyo dondoka kwenye udongo mzuri, ni mbegu ambayo imeanguka kwenye moyo mzuri ambao upo tayari kulipokea neno la Mungu na kulitendea kazi, hasa kuzaa watu katika ufalme wa Mungu.
Kunamambo mengina Unaweza kupanda kwa roho yako na kwa mwili;- kuna vitu unavipata au unapanda katika roho unapo sikiliza Neno la Mungu. Kupanda kwa mwili;- kunamatendo ya mwili unayafanya ambayo hayana faida kwenye roho yako. mwanzo 2:7 mwili wa mwana damu ni mavumbi ya aridhi kwa maana yake unaweza kupanda jambo na likaota kwenye mwili. Ndio maana Mungu alimwambia shetani utakula mavimbi ya ardhi ndio maana ni rahisi kwa shetani kupanda magonjwa kwenye mwili wako.
Mwanzo1:12 miche na itoe mbegu, ambazo mbegu zake zimo ndani. Maana yake ndani ya mbegu moja kuna mapori. Mfano mzuri utaona kwa wakulima wanapanda mbegu moja lakini wana vuna muhindi ambao unapunje elfu moja. Je mtu angekula ile punje ya muhindi, maana yake amekula magunia ya mahindi.
MFANO WA MTUNZA MBEGU KAMA NENO LA MUNGU
Utaona katika Biblia kuna watu ambao Mungu aliwajua toka tumboni na kumwambia Raheli mataifa makubwa mawili yanapigana ndani yako. Mwanzo 25:21- 34 mataifa mawili ndani ya tumbo moja, baadaye walizaliwa kwake watoto mapacha, Yakobo na Essau. Yakobo alikuwa ni mtu ambaye alikuwa anatunza mbegu. Lakini Esau alikuwa ni mwindaji na alikuwa hana uwezo wa kuifazi mbegu, kwasababu  alikuwa akiwinda kwa mshale na kummaliza mnyama. Yakobo alikuwa mkulima ndio maana alikuwa ana tunza mbegu. Utaona kwenye maandiko Essau aliamua kuuza uzaliwa wake wa kwanza kwasababu alikuwa atunzi mbegu kwenye ghala yake. Hakasahau kuwa kuna Baraka ya kuwa mzariwa wa kwanza.  Kwenye Biblia kuna Baraka nyingi za mzariwa wa kwanza lakini kubwa ni hizi:-
BARAKA YA MZALIWA WA KWANZA
                   i.            Baraka ya mzazi
                 ii.            Baraka ya Mungu: Mungu anasema mtoto wa kwanza ni wa Kwangu.
              iii.            Ni mtawala wa familia.
Hatakama umezaliwa maskini ila kwa Baraka za Mungu utafanikiwa.
Essau na Yakobo nani alikuwa Mwizi?
Essau alimwambia Yakobo umeniibia Baraka zangu za uzaliwa wa kwanza, amesahau kwamba alimuuzia uzaliwa wake wa kwanza kwa Yakobo. Kwa maneno mengine kwenye ulimwengu waroho Yakobo alikuwa Essau na Essau alikuwa ni Yakobo. Ndio maana kila mahari Yakobo alipo kwenda alifanikiwa, alipo kuwa kwa Labani alipokuwa anafuga wanyama na wakazaliana sana. Siri ya Yakobo alikuwa anatunza mbegu.
MANENO KAMA MBEGU
Neno la Mungu ni mbegu. Hata maneno ya shetani ni mbegu. Kuna maneno ambayo unajitamkia mwenyewe mabaya yanakuwa ni mbegu kwenye maisha yako. Ndio maana akasema kwenye kitabu cha Yoeri aliye zaifu na aseme mimi ni hodari.
Kanuni ya mbegu ni lazima ioze kabla haija tokea. Maandiko yanasema mbegu isipo anguka chini ya aridhi ikafa haiwezi kumea. Unapo panda mbegu kuna kipindi cha kuishi kwa imani. Kwa mfano ukipanda karanga na kufukia, watu hawata jua hatakama Utaendelea kumwagilia kwasababu ipo chini ya aridhi, lakini unapo zidi kumwagiria ndipo utakapo una imetokea au kuchanua. Lakini wapo wengine wakimwagia wasipoona kitu na hukata tamaa kwa sababu hajaona kitu kinacho onekana pale. Unapo panda mbegu kanuni ya imani inaanza kutumika. Nikama mchungaji akisema poke Biashara kubwa, uanze kuona umepokea kama mbegu. Na uanze kutengeneza picha na kumshukuru BWANA na BWANA atakuinua 2wakorintho4:7 utu wetu wanje unachakaa la kini wa ndani unafanywa upya siku kwa siku. Ishi kwa imani leo ilikesho ukavune. Kunawatu wanakuzalau leo ilakesho watakueshimu kwa jina la YESU. Muhubiri 11:1-6, paangukiapo ule mti papohapo utalala; imani yako inaangukia wapi? Sitakufa bali nitaishi,  anasema asubuhi panda wala usiuzuie mkono wako, wewe panda kila unachokiona baada ya muda utakiona kile ulicho kipanda. Asubuhi panda, jioni panda, usiku panda. Panda kwenye uongozi, utajiri, mifugo, mali na hazina.  Unapokuwa na mbegu usione kama umeshika mbegu ona kama umebeba mapori ya iyo mbegu. Muhubiri 4:14
Unapo panda ukiona mche umetokea anza kuweka na walinzi wa kulinda maana biashara yako, kazi yako, maisha yako yanaenda kuwa mti mkubwa. Kama unacheleani moja anzakuona unachuo cha ushonaji. BWANA akamwambia Abrahimu inua macho yako kuanzia hapo ulipo nchi uonayo nimekupa. Mungu anataka kukutoa kutokea hapo ulipo,, hauwezikuishia hapo kwa jina la Yesu anza kuona ushindi mbele yako kwa Jina la Yesu. Je unaona nini mbele yako leo? Unaona mbegu au unaona pori? Unambegu ndani yako Mungu kaiweka unatakiwa uimwagilie kwa jina la Yesu. Mungu anasema inua macho yako tazama kutokea hapo ulipo anza kuangalia unapo kwenda kwa jina la Yesu
 Watu wanapo kuona maisha yako wana comment maisha yako unayo ishi leo, lakini Bwana anampango mpya na wewe. Heri apandaye kwa machozi atavuna kwa furaha.
Maombi
Baba Mungu katika jina la Yesu Kristo Mwana wa Mungu aliye hai,Napanda ushindi juu ya maisha yangu kwa jina la Yesu, imeandikwa nitakwenda mbele yako na kupasawazisha pale palipo paruza kwa jina la Yesu, Nisafisha njia zangu za mafanikio kwa jina la Yesu. Napanda kuwa wa juu kwenye maisha yangu kwa jina la Yesu maana imeandikwa utakuwa kichwa na wala si mkia. Nakataa kuwa mkia kwa jina la Yesu. Bali najitamkia mafanikio juu ya maisha yangu kwa jina la Yesu.

by Information Ministry

usikose kufuatilia mwendelezo wa masomo mengine ya ufufuo na uzima Arusha yanayo fundishwa na askofu Frank Andrea au ungana nasi live kupitia link :-
·        
·                                                                    
·                                                      
 











Sunday, October 19, 2014

PEPO WALIPUKA IBADA YA SIFA UFUFUO NA UZIMA ARUSHA

Ndani ya nyumba ya ufufuo na uzima ARUSHA, huku Jackson Benty na platform wakimsifu Mungu mashetani yaliyo kuwa ndani ya Dada mmoja yalipuka na Akafunguliwa hapo hapo,, halleluya Yesu atukuzwe

Dada aliyekuwa amekubwa na mashetani

Dada baada ya kufunguliwa

Maelfu katika bonde la ufufuo na uzima ARUSHA wakimchezea MUNGU

ARUSHA YA PINDULIWA CHINI JUU

Kutoka katika Bonde la kukata maneno KAWE, Dar es salamu, Ni yule yule MWANAMAPINDUZI  Pastor MAXIMILIAM MACHUM atua katika Bonde la kukata maneno ARUSHA , Bonde la tikiswa kwa nguvu za MUNGU 

pastor maximilian machumu ndani ya bondela ufufuo na uzima Arusha
                                                                                                                                                         




maelfu ya wakazi wa Arusha wakimshangilia MUNGU na kumsifu, huku mwana mapinduzi akimwimbia Bwana Yesu  wimbo wa bonde la kukata maneno



MWANAMAPINDUZI  ( PASTOR MAXIMILIAN MACHUMU
MAKUTANO YA MAJESHI YA BWANA ARUSHA


maeflu ya watu ufufuo na uzima ARUSHA




















Friday, August 29, 2014

AVULIWA PETE YA JINI MAHABA NA KUVALISHWA PETE YA BWANA YESU


Pastor Frank Andrea akimfungua dada aliye vamiwa na majini mahaba na akumvalisha pete ya Bwana Yesu



Katika nyumba ya ufufuo na uzima Arusha dada aliye fahamika kwa jina la Dorisi Ahadi ambaye aliolewa kwa namna ya rohoni na mahetani( jini mahaba) afunguliwa baada ya kuombewa na Baba yetu mchungaji Frank Andrea. Dorisi anasema alianza kujiwa na mwanaume ndoto mara kwa mara, mwisho akajikuta anafunga ndoa na mtu ambaye hamjui, kumbe toka siku hiyo ndio alikuwa amevalishwa pete, mikufu na bangili za kishetani. Baba yetu akamvalisha PETE ya BWANA yesu rasmi.

Thursday, August 28, 2014

SHETANI KATIKA UZAO WA WANADAMU - Snp Gwajima

IBADA YA TAREHE 17/08/2014
SOMO: SHETANI KATIKA UZAO WA WANADAMU
MCHUNGAJI KIONGOZI JOSEPHAT GWAJIMA
Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima

Shetani ni roho lakini alishahama katika roho na yupo katikati ya wanadamu na unaweza kumkuta mtu anaonekana binadamu kumbe ana roho ya kishetani.  Mafarisayo walipomwendea Yesu katika Mathayo23:33 Yesu aliwaambia 33 Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum?  pia katika kitabu cha Mathayo 12:34 34 Enyi wazao wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake. 35 Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya.  pia kitabu cha Mwanzo 3:15 15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigin. Kwa ufupi kuna wanadamu kabisa tunaishi nao lakini si binadamu kama wanavyoonekana kwa jinsi ya mwili.
Mwanzo19:1-10 Basi, wale malaika wawili wakaja Sodoma jioni; na Lutu alikuwa amekaa mlangoni pa Sodoma. Lutu akawaona akaondoka akaenda kuwalaki, akainama kifudifudi. 2 Akasema, Bwana zangu, karibuni nawasihi mwingie nyumbani mwa mtumwa wenu, mkalale, mkanawe miguu yenu, hata asubuhi mwondoke na mapema mkaende zenu. Wakasema, Sivyo, lakini tutakaa uwanjani usiku kucha. 3 Akawasihi sana, nao wakaja, wakaingia nyumbani mwake. Akawafanyia karamu, akawapikia mikate isiyochachwa nao wakala. 4 Hata kabla hawajalala, watu wa mji, wenyeji wa Sodoma, wakaizunguka nyumba, vijana kwa wazee, watu wote waliotoka pande zote. 5 Wakamwita Lutu, wakamwambia, Wa wapi wale watu waliokuja kwako usiku huu? Uwatoe kwetu, tupate kuwajua.
Lutu alikuwa anaongea na hawa malaika ili wale na wanawe miguu wakati ni malaika na hakujua kama ni malaika, lakini sio watu, malaika hawa Lutu amewaona kana kwamba ni binadamu na walikula chakula na hii inatufundisha kumbe sio kila anayekula umwite mtu lazima ujue kuna uzao usio wa kibinadamu unafanya kazi pamoja na wanadamu na kazi Yetu ni kuuondoa ule uzao  na kujenga Ufalme wa mwanakondoo. Hata wale wenyeji wa mji wa sodoma na gomora waliwadhania kuwa ni watu lakini walikuwa ni malaika.
Waebrania13:2 Msisahau kuwafadhili wageni; maana kwa njia hii wengine wamewakaribisha malaika pasipo kujua.
Hapa tunajifunza kuwa tunaweza kukutana na mtu njiani na kumfadhili kumbe ni malaika wa giza aliye vaa mwili na tunatakiwa tuangalie zaidi ya akili za kibinadamu ili kujua aliye mtu na asiye mtu, sio unakutana na mtu njiani anakuambia anakupenda hapohapo mnachukuana na kwenda nyumbani na baadae mnafunga ndoa na matatizo yanakujia tangu ulipoanza uhusiano na mtu huyo ama wa kibiashara au kimwili lakini kiuhalisia yule alikua ni uzao wa kishetani aliye kuja kwako na kukuletea matatizo.
Kuna binadamu lakini ni mashetani asilimia miamoja wamejichanganya katika uzao wa wanadamu na kufanya mambo ya ajabu lakini wanaonekana ni watu wa kawaida tu kumbe ni mashetani wametumwa toka kuzimu kuja duniani kuharibu mataifa na maisha ya watu. Majini,majoka,mizimu,miungu ya mashariki ya mbali, mapepo wanaitwa malaika wachafu(waovu) wote hao wanaweza kuvaa mwili na kuishi na binadamu makazi yao ni kuzimu ndio hao Biblia inawaongelea kwamba “ni rahisi  kueneza mambo machafu na wanahekima kwa mambo mabaya lakini ni wapuuzi kwa mambo yalio mema” na hao wataangamizwa kwa jina la Yesu. Na malaika wema ni malaika watakatifu wanakaa mbinguni. Malaika wote wanaweza kujigeuza kuwa kitu chochote.
Waebrania1: 7 Na kwa habari za malaika asema, Afanyaye malaika zake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa miali ya moto.
Malaika wetu wa mbinguni wanaweza kugeuka kuwa upepo
Yuda1: 6 Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.
Hawa ni mashetani lakini ni malaika wagiza.
Ufunuo12: 7 Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;
Uzao wa kishetani katikati ya wanadamu na nyakati hizi ni nyakati ambazo mpinga kristo anataka kuingia duniani na atakuwa na mama yake na Baba yake lakini watu hawajui hili kwakua wanajua kila aliye na mwili ni mwanadamu wa kawaida Mfano Yesu alikuwa anajulikana ni mwana wa Yusufu na Mariamu kumbe alikuwa katoka Mbinguni kwenye makao yake na ni mwana wa Mungu Baba wa mbinguni.
Yesu alikutana na mwanamke mmoja kisimani na Yesu alimuuliza kuwa unaye mume? Yule mama alimjibu hapana maana nilio nao ni watano na akajibu sina mume na Yesu akasema umesema vyema, maana yake alikuwa na wanaume ambao wanamharibia maisha yake.
Biblia inasema mpingeni shetani naye atawakimbia na hatutakiwi kuwakimbia watu hawa wenye miili ya kibinadamu waliotoka kuzimu bali tunawafuata huko huko walipo. Na huyu jini au joka anaweza kuwa Mchungaji, Mwanasiasa, Paroko, au mtu yeyote anaongea vizuri lakini sio mtu anamwili wa kibinadamu ndani anaroho ya kishetani.
Namna ambayo hawa mashetani watu wanaweza kumwangamiza mtu
1.       Kwa njia ya macho, mtu anaweza kukuangalia tu ukauua wiki mbili. Kwa kutumia macho yako anakurushia vitu na vinakupata.
2.       Kupitia mahusihano ya kimwili
“1Wakorintho6: 16 Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja.” Biblia inasema mume na mke wanapooana wanakua na uhusihano na uhusihano unaewaleta pamoja na aliye umbwa na kahaba ni mwili mmoja . pia Yesu kristo na sisi kanisa tunauhusiano kupitia Roho mtakatifu. Shetani anapokuwa na uhusihanowa kimwili na mtu lengo lao ni kuwawekea watu matatizo unashangaa bihashara inaanza kuharibika au unashangaa unapatwa na mikosi kumbe ni unakua umejiungamanisha na shetani uliyefanya naye mahusihano. Pia kwenya ndoto unapoota unafanya mahusihano unakuwa unajiungamanisha na mashetani na hapo matatizo yanakua yanaanza na ukifuatilia maisha yako unaona matatizo yako yameanzia pale ulipokutana kimwili na mtu Fulani ambaye ndani yake anakusudi la kishetani.  Pia unapoona mtu anajiuza unadhani ni mtu kumbe ni shetani yupo mawindoni na anapokutana na mtu kimwili anamwachia ushetani ndani yake na mambo yake yanaanza kuharibika na anakua anamilikiwa na nguvu ya kishetani kwenye maisha yake ma mambo yanaanza kuharibika.
ZABURI 78:49 Akawapelekea ukali wa hasira yake, Ghadhabu, na uchungu, na taabu, Kundi la malaika waletao mabaya.
3.       Kupokea zawadi kutoka kwake. Nguvu inaweza kuwa ndani ya kitu ulichopewa na mtu
Matendo ya mitume19: 12 hata wagonjwa wakaletewa leso na nguo zilizotoka mwilini mwake, magonjwa yao yakawaondokea, pepo wachafu wakawatoka. Maana yake kile kinachotoka kwa mtumishi wa Bwana kinabeba uweza wa Bwana na kinaweza kutenda miujiza kwa wagonjwa. Sasa vilevile na mashetani wanaweza wakabeba uweza wa kishetani kwenye vitu na matatizo yakawapata watu mfano mikufu, saa, nguo viatu,gari, au kitu chochote kinakuwa kimebeba uweza wa kishetani  ndani yake kama magonjwa na matatozi mengine” kwa jina la yesu ninaangamiza chochote nilichopewa kama zawadi au nimenunua mimi mwenyewe, kwa jina la Yesu chochote kile kilichopandwa ili kuharibu familia au kazi yangu kama ni kitambaa nakuamuru uteketee, kama ni zawadi nakutetekeza kwa damu ya Mwana Kondoo  ushetani ulioletwa kwa njia ya macho au kwa njia ya zawadi ya aina yeyote naiteketeza kwa jina la Yesu, nateketeza kwa jina la Yesu(unapoomba hivi kwenye ulimwengu wa Roho vinateketea) kwa jina la Yesu naiteketeza kila zawadi niliyopewa na mtu yeyote asiye binadamu aliyekuja kwenye maisha yangu namteketeza kwa jina la Yesu, iwe ni zawadi iliyonuiziwa kifo, balaa, mikosi, naivunja kwa jina la Yesu, kitu chochote kilichonuiziwa manuizo ya kishetani  juu yangu au familia yangu nakiteketeza kwa damu ya mwana kondoo. Namshambulia binadamu yeyote aliyetumwa kuja kufanya mahusihano na mimi na kuniwekea manuizo ya kishetani namshaambulia kwa jina la Yesu, kwa damu ya mwanakondoo, aliyenitupia mishale kwa njia ya macho,  chakula,  maji  ninaiharibu kwa damu ya mwanakondoo, kwa jina la Yesu ushetani wowote uliotumwa ndani yangu naukataa kwa jina la Yesu.  Jini wa uchawi aliye tumwa kwangu kwa njia ya kishetani na balaa na mikosi iliyopangwa juu yangu naivunja kwa jina la Yessu na kifo kilichopangwa juu yangu nakifuta kwa damu ya mwanakondoo. Sitakufa kwa jina la Yesu, kifo chochote kilichopangwa juu yangu nakivunja kwa jina la yesu.  Navunja tamaduni zote za kishetani  kwa jina la Yesu.
 AMEN.